JUA JINSI YA KUPIKA

leo tutaenda kujifunza jinsi ya kupika mchemsho wa viazi,ndizi na nyama.

mahitaji

  • Ndizi mbichi 15
  • Nyama ya ng'ombe ( kilo moja)
  • Viazi mviringo 6
  • Kitunguu swaumu
  • Tangawizi
  • Kitunguu maji
  • Nyanya 1 kubwa
  • Mafuta (vegetable oil)
  • Chumvi
  • Limao
  • Pilipili
Matayarisho

1.Chemsha nyama
 2. limao 
endelea

 kitunguu swaum, tangawizi chumvi na maji kiasi mpaka nyama iive, Hakikisha unaiacha na supu kiasi kwa ajili ya kuwekea kwenye ndizi.Kisha katakata nyanya na vitunguu na uweke pembeni .Menya ndizi na viazi kisha zichemshe pamoja na vitunguu, nyanya, maji kidogo, mafuta  na uhakikishe haziivi kabisa. Baada ya hapo tia nyama na supu yake, pilipili mzima na chumvi na uache uchemke mpaka ndizi na viazi viive.Na baada ya hapo mchemsho wako utakuwa tayari kwa kuliwa

No comments:

Namna ya kupika Vitumbua Vitumbua ni aina ya vitafunwa vya chai ambavyo hutengenezwa kwa kutumia unga wa mchele. Kiasili vitumbua ni ch...